"Tunaungwa mkono vizuri sana, tunaunganishwa na kiswahili, leo mazungumzo yote yamekwenda kwa Kiswahili na ni kizuri kabisa, leo tumetumia neno 'tunakwenda kuweka saini mikataba', hatukusema 'tunaenda kuweka kidole mikataba...".Rais Samia. #ZiaraUhuruKenyatta.
December 10, 2021
#KIMATAIFA:Idadi ya vifo kufuatia ajali ya lori lililokuwa limebeba wahamiaji haramu Kusini mwa Mexico yafikia 54 huku majeruhi wakiwa 105. Lori hilo lilipinduka baada ya kupoteza muelekeo na kugonga daraja la watembea kwa miguu.
December 10, 2021
#HABARI: Jeshi la Polisi mkoani Lindi, limemfuta kazi askari No.H.2324 PC Joseph kwa kosa la kumpiga risasi askari mwenzake No J.1752 PC Onesmo Joseph wakiwa lindo katika Benki ya CRDB Tawi la Ruangwa kilichosababisha kifo chake akiwa njiani kupelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoani Lindi ACP Mtatiro Kitinkwi .
December 10, 2021
#HABARI: Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam limepiga marufuku kwa mtu yeyote asiyehusika na mambo ya kiusalama kuingia uwanjani na silaha yoyote ikiwemo silaha za moto, visu, Panga au mawe katika mchezo wa watani wa jadi Simba na Yanga Disemba 11, 2021 .
December 10, 2021
#ITVMagazeti:Makomando wanogesha sherehe za Uhuru Dar / Ni 60 ya viwango, Desemba 10, 2021.
December 10, 2021
Similar accounts
Disclaimer
The data provides is not authorized by TikTok. We are not an official partner of TikTok.
Use of materials from the resource is permitted only with a link to our resource.
Contact