*PONGEZI KWAKO NDUGU HAKAINDE HICHILEMA, RAIS MTEULE WA ZAMBIA* *_Taarifa ya Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya ACT Wazalendo ikimpongeza Ndg. Hakainde Hichilema kwa kuchaguliwa kuwa Rais mpya wa Jamhuri ya Zambia._* Kwa kuzingatia matokeo rasmi yaliyokwishatangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Zambia (ECZ) na baada ya Rais Edgar Lungu kukiri kushinwa ni dhahiri kuwa Ndg. Hakainde Hichilema ambaye ni mgombea wa chama cha UPND amevuka wigo wa zaidi ya asilimia 50 (50%+1) ya kura zote na hivyo kushinda uchaguzi mkuu na kumuacha mbali mgombea aliyekuwa akitetea nafasi hiyo ya Urais, Ndg. Edgar Chagwa Lungu. Sisi ACT Wazalendo tukiwa ni Chama kiongozi wa Upinzani nchini Tanzania na Chama rafiki wa Chama cha UPND, tunampongeza Ndg. Hakainde Hichilema kwa kuchaguliwa Rais wa 7 wa Jamhuri ya Zambia. Ni matumaini yetu kuwa, chini ya uongozi wa Hakainde Hichilema, nchi zetu mbili- Tanzania na Zambia, zitashamirisha na kuimarisha uhusiano wa kihistoria katika nyanja za kiuchumi, miundombinu, na kikanda kupitia Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC). Tunakutakia mafanikio katika majukumu yako mapya ya kuitumikia Zambia na hivyo kutimiza matakwa ya wananchi wa Zambia. Hongera sana kamaradi HH. _Imetolewa na:_ *Fatma Abdulhabib Ferej* *Mkuu wa Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,* *ACT Wazalendo,* *Dar es salaam,* *Tanzania.* *15 Agosti, 2021.* *Simu: +255 713 052 428* *+255 777 424 390*
August 17, 2021
Siasa zilizo bora ni siasa za USHAWISHI (persuasive politics). Ugumu tunaoupata Tanzania ni namna ya kufanya siasa bila KUHASIMIANA au KUGAWA watu. CHUKI CHUKI CHUKI. Mwenye mawazo tofauti sio ADUI. Anawaza tofauti na wewe tu. HATUKUI? HATUTAFAKARI?
July 05, 2021
Last 8 predictions: Denmark, Italy, Netherlands, Belgium, Spain, France, England and Sweden.
June 24, 2021
Wakati umewadia. Mlisubiri sana sehemu ya mwisho ya mazungumzo yangu ya mwisho na Tundu Lissu haya hapa. Kwanini nilihama Chadema? Niliunda ACT kukomoa CDM? etc #nowplaying Speaking out with Tundu Lissu by NADJ feat. Zitto Kabwe Sehemu ya 3 na ya mwisho bofya LINK kwenye BIO hapo juu via @audiomack
June 23, 2021
Fuatilia *Azam TV #UTV Channel #108 "MIZANI YA WIKI"* Leo SAA mbili na nusu usiku (20:30 Hrs) Balozi Ami Mpungwe na Balozi Getruda Mongella Mwanasiasa mkongwe pamoja na Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe na Theddy Ladislaud Mshauri wa Rais Edigar Lungu katika masuala ya mawasiliano ya kimkakati *****_Wakijadili maisha ya mwendazake Rais wa kwanza wa Zambia Kenneth Kaunda* * ***_ Mjadala utaongozwa hewani na Mtangazaji wa Azam Tv Bw. Faraja Sendegeya. Karibu
June 21, 2021
Jumatatu kuanzia Saa moja Asubuhi nitakuwa #JotoKali na @Gerald_Hando ambapo pia nitachambua mambo mbalimbali kuhusu Bajeti ya Serikali Mwaka 2021/2022 na masuala mengine mengi @EfmTanzania
June 20, 2021
Nilikuwa Nina interview nzuri sana Jana chumba cha Habari cha @MwananchiNews @TheCitizenTZ kuhusu Bajeti ya Serikali ya Mwaka 2021/2022. Nataraji mjadala utakuwa bora zaidi ili kuwezesha mabadiliko muhimu yanayotakiwa. Asante sana Wahariri wa Mwananchi na The Citizen
June 20, 2021
Similar accounts
Disclaimer
The data provides is not authorized by TikTok. We are not an official partner of TikTok.
Use of materials from the resource is permitted only with a link to our resource.
Contact