Unauzungumziaje usajili wa Makambo akimaliza na @yangasc ? #TimesFMDigital #TimesFmNiBaraka #HujasikiaBado #mgusowajamii📻🎧🎤🔥🔥🔥
August 01, 2021
Straika wa zamani wa @yangasc , Makambo ameshawasili Tanzania kwa ajili ya kukamilisha mchakato wa kujiunga na timu hiyo. #sports #michezo #mpira #makambo #soka #usajili
August 01, 2021
RAISI SAMIA AIPONGEZA TIMU YA TAIFA U23 KWA UBINGWA WA CECAFA 2021 Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameipongeza timu ya taifa ya vijana kwa kutwaa ubingwa wa Cecafa 2021 kwa vijana walio chini ya umri wa miaka 23. Kupitia ukurasa wake wa Twitter Rais Samia ameandika: "Nawapongeza timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 23 kwa kutwaa ubingwa wa mashindano ya Afrika Mashariki na Kati (CECAFA 2021). Ushindi huu ni heshima kwa nchi yetu na ni chachu ya kukuza michezo. Natoa wito kwa wadau wa michezo kuendeleza jitihada za kukuza michezo yetu." @scopeboiii @wizara_elimutanzania @ikulu_mawasiliano
August 01, 2021
Klabu ya Yanga SC imetangaza kumsajili mshambuliaji Fiston Mayele kutoka AS Vita. @yangasc @kessysports_tz @tanfootball @mayelefiston #usajili #soka #yanga
August 01, 2021
KAGAME CUP: Yanga wakiwasili Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Ni Yanga SC dhidi ya Nyasa Big Bulltes kutoka Malawi kuanzia saa 1:00 usiku. #Yanga @TFF #KagameCup #KagameCup2021 #CecafaKagameCup #CecafaKagameCup2021
August 01, 2021
KAGAME CUP: Big Bulletes wakiwasili Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Ni Yanga SC dhidi ya Nyasa Big Bulltes kutoka Malawi kuanzia saa 1:00 usiku, leo Jumapili. #Yanga @TFF #KagameCup #KagameCup2021 #CecafaKagameCup #CecafaKagameCup2021
August 01, 2021
DONALD TRUMP: MARUFUKU MAREKANI Siku kama ya leo mwaka mmoja uliopita, aliyekuwa Rais wa 45 wa Marekani, Donald Trump alitoa tamko la kutaka kuufungia mtandao wa Tiktok wa nchini China ndani ya Marekani. Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa safari yake akirejea mjini Washington DC akitokea Florida alisema kuwa kwa kadri ambavyo mtandao huo unazidi kutumika nchini humo ndivyo ambavyo hati hati ya kuufungia inaongezeka. "Kampuni ya Tiktok tunaipiga marufuku Marekani," Trump aliwaambia waandishi wa habari. Moja kati ya sababu za kutaka kuufungia mtandao huo ni kwamba, maafisa wa usalama wa nchini Marekani walionesha wasiwasi kwamba programu hiyo ya Kampuni ya ByteDance ya China, inaweza kutumiwa kukusanya data binafsi za raia wa Marekani. Japokuwa TikTok ilikanusha madai ya kwamba inadhibitiwa au inashirikisha data zake na Serikali ya China. Inasemekana kwamba Kampuni ya Microsoft imekuwa ikifanya mazungumzo ya kununua programu hiyo kutoka kwa Kampuni ya ByteDance, japokuwa Trump alionekana kutilia mashaka makubaliano hayo kama yangeweza kufanyika. Na kama makubaliano hayo yangefanyika, taarifa zinasema kwamba ByteDance isingekuwa na umiliki wowote wa programu hiyo kwa nchini Marekani. Kwa sasa chini ya tawala ya Rais wa 46 wa Marekani, Joe Biden, mtandao huo unaendelea kutumika bila vikwazo vya hapa na pale, kwa mujibu wa sheria. #TimesFMDigital #TimesFmNiBaraka #HujasikiaBado #MgusoWaJamii
August 01, 2021
WAZIRI MKUU ATEMBELEA SHAMBA NA KIWANDA CHA PARACHICHI RUNGWE WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea shamba la parachichi na kiwanda cha kuchakata mazao ya parachichi na kuwasisitiza wananchi walime zao hilo kwa kuwa faida yake ni kubwa. Ametembelea shamba hilo leo (Jumapili, Agosti 1, 2021) katika Kijiji cha Ilolo, Wilaya ya Rungwe, Mbeya na linamilikiwa na Kampuni ya Kuza Africa na Moravian Farming PVT. “Kilimo cha parachichi kina manufaa makubwa sana, wananchi ongezeni ukubwa wa mashamba ya parachichi na Serikali italisimamia kuanzia hatua za maandalizi ya shamba hadi masoko," alisema. Waziri Mkuu ameziagiza Halmashauri zote zinazolima zao la parachichi zianzishe vitalu vya kuotesha miche na kuigawa kwa wakulima ili kuhamasisha wananchi wengi kulima zao hilo. Amesema zao la parachichi ni miongoni mwa mazao yenye faida kubwa na linazalishwa kwa gharama nafuu, hivyo amewahimiza wananchi kulima zao hilo kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi. Naye, Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amewapongeza wawekezaji hao kwa kuwa wamewezesha wakulima kutatua changamoto ya soko la uhakika wa zao la parachichi. Naibu Waziri huyo amesema mbali na kupatikana kwa soko la parachichi katika kiwanda hicho pia Serikali itahakikisha soko la parachichi za Tanzania nchini Afrika Kusini linafunguliwa. @owm_tz @ikulu_habari @ikulu_mawasiliano @jaffarhaniu @vanmohamed
August 01, 2021
ZIARA YA RAIS SAMIA RWANDA Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kesho tarehe 02/08/2021 anatarajia kufanya ziara ya kiserikali ya siku mbili nchini Rwanda baada ya kupewa mualiko na Rais wa nchi hiyo, Paul Kagame. Pia katika ziara hiyo Rais Samia atafanya mazungumzo na mwenyeji wake huyo na kushuhudia utiaji saini wa hati ya makubaliano. Ziara hiyo imelenga kuimarisha uhusiano na ushirikiano baina ya Rwanda na Tanzania.
August 01, 2021
Wanaopewa kipaumbele cha kwanza kwenye mchakato wa kupata chanjo ya kuzuia maambukizi ya Corona. @wizara_afyatz @tanfootball @basata.tanzania @salim_kikeke @wizara_elimutanzania @vanmohamed @jaffarhaniu @samia_suluhu_hassan @ikulu_habari @ikulu_mawasiliano
August 01, 2021
Similar accounts
Disclaimer
The data provides is not authorized by TikTok. We are not an official partner of TikTok.
Use of materials from the resource is permitted only with a link to our resource.
Contact