class="content__text" Rais Samia Suluhu amesema Tanzania itakuwa mwenyeji wa Mkutano wa Kilele cha Jukwaa la Kijani utakaofanyika Septemba 4-8, 2023 unaolenga kujadili mifumo ya chakula barani Afrika. Amezungumza katika Mkutano wa 36 wa Umoja wa Afrika (AU) jijini Addis Ababa nchini Ethiopia.
February 18, 2023
class="content__text" Rais Samia Suluhu akizungumza kwenye mkutano wa 36 wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika katika ukumbi wa Nelson Mandela uliopo Makao Makuu ya umoja huo Jijini Addis Ababa nchini Ethiopia.
February 18, 2023
class="content__text" Linapokuja suala la kununua miwani, kuamua saizi ya uso wako na umbo ni muhimu kwa sababu itakusaidia kupata miwani ya jua inayofaa zaidi kulingana na aina ya uso wako. Miwani ya jua inayofaa inaweza kukupa mwonekano maridadi. Ili kupata miwani bora zaidi ya uso wako, utahitaji kupima uso wako, kuamua umbo la uso wako, na kulinganisha umbo hilo na mtindo wa miwani ya jua.
February 18, 2023
class="content__text" Mchezaji wa Hatayspor ya Uturuki, Christian Atsu amekutwa amefariki chini ya kifusi cha nyumba yake, takribani wiki mbili baada ya tetemeko la ardhi, wakala wake amethibitisha. Atsu ambaye ni raia wa Ghana amewahi pia kucheza Chelsea, Everton, New Castle United na Bournemouth.
February 18, 2023
class="content__text" Watu watatu akiwemo mama mjamzito wameuawa katika kitongoji cha Kilimahewa, kata ya Ludete katika mji mdogo wa Katoro mkoani Geita ambapo wawili wanasadikiwa kuwa ni majambazi waliovamia familia ya Msafiri Renatusi usiku wa kuamkia leo. Tukio hilo limetokea majira ya saa mbili usiku ambapo mama mjamzito aliyetambulika kwa jina la Elinata Elias (27) ameuawa kwa kuchinjwa shingo na kitu chenye ncha kali huku baba wa familia hiyo, Msafiri Renatus akijeruhiwa vibaya. Mashuhuda wa tukio hilo wamesema majambazi hao, akiwemo mtoto wa kiume wa Msafiri Renatus aliyetambulika kwa jina la Jackson Msafiri (25) akiwa na rafiki ambaye jina lake halijafahamika walifika katika familia hiyo na kutekeleza mauaji ya mama huyo. Baada ya kutekeleza mauji hayo majambazi hao waliuawa na wananchi wenye hasira kali waliokuwa na silaha za jadi ambao walikuwa wamezingira nyumba ya Msafiri.
February 18, 2023
Similar accounts
Disclaimer
The data provides is not authorized by TikTok. We are not an official partner of TikTok.
Use of materials from the resource is permitted only with a link to our resource.
Contact